Yesu Ajaribiwa Na Shetani

Kisha Yesu akaongozwa na Roho Mtakatifu mpaka nyikani ili akajaribiwe na shetani. Akakaa huko siku arobaini akifunga, pasipo kula kitu cho chote mchana na usiku, hatimaye akaona njaa. Ndipo shetani akamjia akamwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, amuru mawe haya yawe mikate.”

Mungu, amuru mawe haya yawe mikate.”

Lakini Yesu akamjibu, “Imeandikwa, ‘Mtu hataishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno analotamka Mungu.’ ”

Ndipo shetani akampeleka Yesu mpaka mji mtakatifu wa Yerus alemu, akamweka juu ya mnara wa Hekalu, akamwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu jitupe chini; kwa kuwa imeandikwa, ‘Atawaagiza malaika wake wakuhudumie,’ na, ‘Watakuinua juu mikononi mwao ili usijikwae mguu wako kwenye jiwe.’ ”

Yesu akamjibu, “Pia imeandikwa, ‘Usimjaribu Bwana Mungu wako.’ ”

Kwa mara nyingine shetani akamchukua Yesu mpaka kwenye kilele cha mlima mrefu akamwonyesha milki zote za dunia na fahari zake, kisha akamwambia, “Nitakupa hivi vyote kama ukipiga magoti na kuniabudu.”

10 Yesu akamwambia, “Ondoka hapa shetani! Kwa maana imean dikwa, ‘Utamwabudu Bwana Mungu wako na utamtumikia yeye peke yake.’ ” 11 Ndipo shetani akamwacha, na malaika wakaja wakamhu dumia.

Yesu Aanza Kuhubiri

12 Yesu aliposikia kwamba Yohana Mbatizaji alikuwa ameka matwa na kuwekwa gerezani, alirudi Galilaya. 13 Akaondoka Nazareti akaenda kuishi Kapernaumu karibu na ziwa, katika eneo la Zabuloni na Naftali. 14 Utabiri wa nabii Isaya ukatimia, kama alivyosema: 15 “Nchi ya Zabuloni na nchi ya Naftali, kuelekea baharini, ng’ambo ya Yordani, Galilaya ya watu wa mataifa - 16 watu wale waishio katika giza wameona nuru kuu; na kwa wale wanaoishi katika nchi ya giza la mauti, nuru imewaangazia.” 17 Tangu wakati huo, Yesu alianza kuhubiri akisema: “Tubuni, kwa maana Ufalme wa mbinguni umekaribia.”

Yesu Awaita Wanafunzi Wanne

18 Yesu alipokuwa akitembea kando kando ya ziwa la Galilaya aliwaona ndugu wawili, Simoni ambaye aliitwa Petro na Andrea ndugu yake. Walikuwa katika mashua wakitupa nyavu zao baharini kwa maana wao walikuwa wavuvi.

19 Yesu akawaambia, “Nifuateni, nami nitawafanya muwe wavuvi wa watu.” 20 Wakaziacha nyavu zao mara moja, wakamfuata.

21 Alipoendelea mbele kidogo, aliwakuta ndugu wengine wawili, Yakobo na Yohana, wakiwa wamekaa kwenye mashua pamoja na baba yao Zebedayo wakishona nyavu zao; akawaita. 22 Wakaacha nyavu zao mara moja, wakamfuata.

Yesu Ahubiri Na Kuponya Wagonjwa

23 Yesu alizunguka Galilaya yote, akifundisha katika masi nagogi na kuhubiri Habari Njema ya Ufalme wa mbinguni, na kupo nya kila ugonjwa na kila udhaifu. 24 Kwa hiyo sifa zake zilienea sehemu zote za Siria. Nao wakamletea wagonjwa wote, waliosumbu liwa na maradhi mbalimbali na maumivu, watu waliopagawa na mashe tani, wenye kifafa na waliopooza, naye akawaponya.

25 Umati mkubwa wa watu ukamfuata kutoka Galilaya, Dekapoli, Yerusalemu, Yudea na kutoka ng’ambo ya mto Yordani.

Yesu Ajaribiwa na Shetani

(Mk 1:12-13; Lk 4:1-13)

Kisha Roho Mtakatifu akamwongoza Yesu hadi nyikani ili akajaribiwe na Shetani. Baada ya Yesu kufunga kwa siku arobaini mchana na usiku, akaumwa njaa sana. Mjaribu[a] akamwendea na akasema, “Ikiwa wewe ni Mwana wa Mungu, basi yaamuru mawe haya yawe mikate.”

Yesu akajibu, “Maandiko yanasema, ‘Mtu hataishi kwa mkate tu, ila kwa kila Neno linalotoka katika kinywa cha Mungu.’”(A)

Kisha Shetani alimwongoza Yesu mpaka mji mtakatifu wa Yerusalemu na akamweka juu ya mnara wa Hekalu. Akamwambia Yesu, “Ikiwa wewe ni Mwana wa Mungu, jirushe mpaka chini! Kwani Maandiko yanasema,

‘Mungu atawaamuru malaika zake wakusaidie,
na mikono yao itakupokea,
    ili usije ukajikwaa mguu wako kwenye jiwe.’”(B)

Yesu akamjibu, “Pia, Maandiko yanasema, ‘usimjaribu Bwana Mungu wako.’”(C)

Kisha Shetani akamwongoza Yesu mpaka kwenye kilele cha mlima ulio mrefu sana na kumwonyesha falme zote za ulimwengu na vitu vya kupendeza vilivyomo ndani. Shetani akamwambia Yesu, “Ukiinama na kuniabudu, nitakupa vitu hivi vyote.”

10 Yesu akamjibu Shetani akamwambia, “Ondoka kwangu Shetani! Kwani Maandiko yanasema, ‘Umwabudu Bwana Mungu wako na umtumikie yeye peke yake!’”(D)

11 Baada ya hayo, Shetani akamwacha. Ndipo malaika wakaja kumhudumia.

Yesu Aanza Kazi yake Galilaya

(Mk 1:14-15; Lk 4:14-15)

12 Yesu aliposikia kuwa Yohana alikuwa amefungwa gerezani, alirudi katika wilaya ya Galilaya. 13 Lakini aliondoka Nazareti. Alikwenda kuishi Kapernaumu, mji ulio kando kando ya Ziwa Galilaya katika eneo la Zabuloni na Naftali. 14 Hili lilitokea ili kutimiza maneno aliyosema nabii Isaya:

15 “Sikilizeni, enyi nchi ya Zabuloni na Naftali,
    nchi iliyo kando ya barabara iendayo baharini,
    ng'ambo ya Mto Yordani!
    Galilaya, wanapokaa Mataifa.
16 Watu wanaoishi katika giza ya kiroho,
    nao wameiona nuru iliyo kuu.
Nuru hiyo imeangaza kwa ajili yao wale
    wanaoishi katika nchi yenye giza kama kaburi.”(E)

17 Tangu wakati huo Yesu alianza kuwaambia watu ujumbe wake unaosema, “Mbadili mioyo yenu na maisha yenu pia, kwa sababu Ufalme wa Mungu umewafikia.”

Yesu Achagua Baadhi ya Wafuasi

(Mk 1:16-20; Lk 5:1-11)

18 Yesu alipokuwa akitembea kando ya Ziwa Galilaya, aliwaona ndugu wawili, Simoni, aitwaye Petro na nduguye aitwaye Andrea. Ndugu hawa walikuwa wavuvi na walikuwa wanavua samaki kwa nyavu zao. 19 Yesu akawaambia, “Njooni, mnifuate, nami nitawafanya kuwa wavuvi wa aina nyingine. Nitawafundisha jinsi ya kukusanya watu badala ya samaki.” 20 Mara moja, Simoni na Andrea wakaziacha nyavu zao na kumfuata Yesu papo hapo.

21 Yesu akaendelea kutembea kutoka pale. Akawaona ndugu wengine wawili, Yakobo na Yohana wana wa Zebedayo. Walikuwa kwenye mashua pamoja na Zebedayo baba yao. Walikuwa wakiandaa nyavu zao za kuvulia samaki. Yesu akawaita wamfuate. 22 Mara moja wakaiacha mashua pamoja na baba yao na wakamfuata Yesu.

Yesu Afundisha na Kuponya Watu

(Lk 6:17-19)

23 Yesu alikwenda sehemu zote za Galilaya, akifundisha na akihubiri Habari Njema katika masinagogi kuhusu Ufalme wa Mungu. Aliponya magonjwa yote na madhaifu mengi ya watu. 24 Habari kuhusu Yesu zilienea katika nchi yote ya Shamu, na watu waliwaleta wale wote wenye kuteswa na magonjwa na maumivu mbalimbali. Baadhi yao walikuwa na mashetani, wengine walikuwa na kifafa na wengine walikuwa wamepooza. Yesu akawaponya wote. 25 Makundi makubwa ya watu walimfuata; watu kutoka Galilaya, na jimbo lililoitwa Miji Kumi,[b] Yerusalemu, Yuda na maeneo ng'ambo ya Mto Yordani.

Footnotes

  1. 4:3 Mjaribu Kwa maana ya kawaida, “Shetani”.
  2. 4:25 Miji Kumi Jimbo hili lilikuwa mashariki ya Ziwa la Galilaya na wakazi wake hawakuwa Wayahudi. Miji Kumi imejulikana pia kama Dekapoli.