Yesu Ahudhuria Sikukuu Ya Vibanda Yerusalemu

Baada ya mambo haya, Yesu alikwenda sehemu mbalimbali za Galilaya. Aliamua kutokwenda Yudea kwa sababu Wayahudi huko wali taka kumwua. Sikukuu ya Vibanda ilipokaribia, ndugu zake Yesu walimwambia, “Ni vema utoke hapa uende Yudea ili wanafunzi wako wapate kuona miujiza unayofanya. Mtu anayetaka kujulikana, hafanyi mambo yake kwa siri. Kwa kuwa unafanya mambo haya, jion yeshe kwa ulimwengu.” Hata ndugu zake hawakumwamini.

Yesu akawajibu, “Wakati wangu wa kwenda huko haujafika. Ninyi mnaweza kwenda wakati wo wote. Ulimwengu hauwachukii ninyi lakini unanichukia mimi kwa sababu ninawashuhudia kwamba matendo yao ni maovu. Ninyi nendeni kwenye sikukuu, lakini mimi sitahudhuria sikukuu hii kwa sababu wakati wangu haujawadia.” Baada ya kusema hivyo, akabaki Galilaya. 10 Lakini ndugu zake walipokwisha kuondoka kwenda kwenye sikukuu, yeye pia alikwenda kwa siri. 11 Huko kwenye sikukuu viongozi wa Wayahudi walikuwa wakimtafuta na kuulizana, “Yuko wapi?”

12 Kulikuwa na minong’ono iliyoenea kumhusu Yesu. Baadhi ya watu walisema, “Ni mtu mwema” na wengine wakasema, “Sio, ana wadanganya watu.” 13 Lakini hakuna aliyemsema wazi wazi maana wote waliwaogopa viongozi wa Wayahudi.

Yesu Atangaza Mamlaka Yake

14 Katikati ya sikukuu, Yesu alikwenda Hekaluni akaanza kuwafundisha watu. 15 Viongozi wa Wayahudi walistaajabia mafund isho yake wakasema, “Amefahamuje mambo haya naye hakusoma?”

16 Yesu akawajibu , “Mafundisho yangu hayatoki kwangu. Yanatoka kwake yeye aliyenituma. 17 Mtu ye yote akipenda kufanya mapenzi ya Mungu, atajua kama mafundisho yangu yanatoka kwa Mungu au ninasema kwa mamlaka yangu mwenyewe. 18 Mtu anayesema kwa mamlaka yake mwenyewe hufanya hivyo kwa kutaka kujitukuza. Lakini mtu anayetafuta kumtukuza Mungu aliyemtuma, ni mwaminifu na hana udhalimu wo wote. 19 Kwani Musa hakuwapeni sheria? Mbona hakuna hata mmoja wenu anayetii sheria? Kwa nini mnataka kuniua?”

21 Yesu akawajibu, “Nimefanya muujiza mmoja na nyote mkas taajabu. 22 Lakini kwa kuwa Musa aliwaamuru kutahiri watoto wenu wa kiume, ingawa kwa kweli si Musa aliyeanzisha desturi hii ila ni mababu zenu, mnamtahiri mtoto hata siku ya sabato. 23 Ikiwa mtu aweza kutahiriwa siku ya sabato kusudi sheria ya Musa isi vunjwe, kwa nini mnanikasirikia kwa kumfanya mtu kuwa mzima kabisa siku ya sabato? 24 Msitoe hukumu kwa kuangalia mambo juu juu. Hukumuni kwa haki.”

25 Baadhi ya wakazi wa Yerusalemu wakasemezana, “Tazameni, huyu si yule mtu wanayetaka kumwua? 26 Mbona anazungumza hadhar ani na wala hawasemi lo lote? Je, inawezekana wanafahamu kwa kweli kama yeye ndiye Kristo? 27 Lakini huyu mtu tunafahamu ana kotoka, nasi tunajua ya kuwa Kristo atakapokuja hakuna atakayefa hamu atokako.”

28 Yesu, akiendelea kufundisha Hekaluni, akatangaza kwa sauti, “Hivi kweli mnanifahamu na kufahamu ninakotoka? Mimi sikuja kwa mamlaka yangu mwenyewe. Yeye aliyenituma ni wa kweli na wala ninyi hamumjui. 29 Lakini mimi namjua kwa kuwa nimetoka kwake, na ndiye aliyenituma.”

30 Basi viongozi wa Wayahudi wakajaribu kumkamata, lakini hakuna aliyethubutu kumshika kwa sababu wakati wake ulikuwa bado haujatimia.

31 Watu wengi kati ya wale waliokuwepo, walimwamini, wakasema, “Hivi Kristo akija, atafanya miujiza mikuu zaidi kuliko aliyoifanya huyu?”

Walinzi Wanatumwa Kumkamata Yesu

32 Mafarisayo waliposikia minong’ono hii, wao pamoja na makuhani wakuu, waliwatuma walinzi wa Hekalu waende kumkamata.

33 Yesu akasema, “Bado niko nanyi kwa muda mfupi, kisha nitarudi kwake aliyenituma. 34 Mtanitafuta lakini hamtaniona kwa kuwa huko nitakapokuwa, ninyi hamwezi kufika.” 35 Basi viongozi wa Wayahudi wakaulizana, “Huyu mtu anataka kwenda wapi ambapo hatuwezi kumpata? Au anataka kwenda katika miji ya Wagiriki ambapo baadhi ya watu wetu wametawanyikia, akawafundishe Wagiriki 36 Ana maana gani anaposema, ‘Mtanitafuta lakini hamtaniona, na huko nitakapokuwa ninyi hamwezi kufika ?”’

Vijito Vya Maji Yaletayo Uzima

37 Siku ya mwisho ya sikukuu, ambayo kwa kawaida ndio ili kuwa kilele cha sherehe, Yesu alisimama akasema kwa sauti kuu, “Mtu ye yote mwenye kiu na aje kwangu anywe. 38 Kama Maandiko yasemavyo, ye yote aniaminiye, vijito vya maji yaletayo uzima vitatiririka kutoka moyoni mwake.” 39 Yesu alisema haya kuhusu Roho Mtakatifu ambaye wote waliomwamini Yesu wangempokea, kwani mpaka wakati huo, Roho alikuwa bado hajatolewa, kwa kuwa Yesu alikuwa bado hajainuliwa na kutukuzwa.

40 Waliposikia maneno hayo, baadhi ya watu walisema, “Hakika huyu ndiye yule Nabii.” 41 Wengine wakasema, “Huyu ni Masihi!” Lakini wengine wakauliza, “Kwani Masihi kwao ni Gali laya? 42 Je, Maandiko hayakusema kuwa Masihi atakuwa mzao wa Daudi na kwamba atazaliwa Bethlehemu, mji alioishi Daudi?” 43 Kwa hiyo kukawa na mgawanyiko kati ya watu kumhusu Yesu. 44 Baadhi yao walitaka kumkamata, lakini hakuna aliyethubutu kumgusa.

Kutokuamini Kwa Viongozi Wa Wayahudi

45 Hatimaye wale walinzi wa Hekalu waliokuwa wametumwa kum kamata Yesu, walirudi kwa makuhani wakuu na Mafarisayo. Wakauli zwa, “Mbona hamkumleta ?”

46 Wale walinzi wakajibu, “Hakuna mtu ambaye amewahi kufundisha kama yeye.” 47 Mafarisayo wakajibu, “Ameweza kuwa danganya hata ninyi? 48 Je, mmewahi kuona kiongozi ye yote au mmoja wa Mafarisayo ambaye amemwamini? 49 Lakini huu umati wa watu wasiojua sheria ya Musa, wamelaaniwa.”

50 Ndipo Nikodemo, yule aliyemwendea Yesu siku moja, ambaye alikuwa kati yao akauliza, 51 “Je, sheria zetu zinaturuhusu kumhukumu mtu kabla ya kumsikiliza na kufahamu alilotenda?”

52 Wakamjibu, “Je, wewe pia unatoka Galilaya? Chunguza Maandiko nawe utaona kwamba hakuna nabii anayetokea Galilaya!” [ 53 Kisha wakaondoka, kila mtu akarudi nyumbani kwake.

Yesu na Ndugu Zake

Baada ya hayo, Yesu alitembea kuizunguka miji ya Galilaya. Hakutaka kutembelea Uyahudi, kwa sababu viongozi wa Kiyahudi kule walitaka kumuua. Huu ulikuwa ni wakati wa sherehe za sikukuu ya Wayahudi ya Vibanda. Hivyo ndugu zake wakamwambia, “Unapaswa kuondoka hapa na kwenda kwenye sikukuu Uyahudi. Kisha wafuasi wako kule wataweza kuona ishara unazofanya. Ikiwa unataka kujulikana, basi usiyafiche mambo unayoyafanya. Ikiwa unaweza kufanya mambo ya ajabu hivi, acha ulimwengu wote uone.” Ndugu zake Yesu walisema hivi kwa kuwa hata wao hawakumwamini.

Yesu akawaambia, “Wakati unaonifaa kufanya hivyo haujafika, lakini kwenu ninyi kila wakati unafaa. Ulimwengu hauwezi kuwachukia ninyi. Bali ulimwengu unanichukia mimi kwa sababu nawaambia watu ulimwenguni ya kwamba wanafanya maovu. Hivyo ninyi nendeni kwenye sikukuu. Mimi sitaenda sasa, kwa sababu wakati unaonifaa haujafika.” Baada ya Yesu kusema hayo, akabaki Galilaya.

10 Ndugu zake nao wakaondoka kwenda kwenye sikukuu ya Wayahudi ya Vibanda. Baada ya kuondoka kwao Yesu naye akaenda huko, ingawa hakutaka watu wamwone. 11 Baada ya sikukuu ile kupita viongozi wa Kiyahudi wakawa wanamtafuta Yesu. Wakasema, “Yuko wapi huyo Yesu?”

12 Lilikuwepo kundi la watu wengi mahali pale. Wengi kati yao walikuwa wakizungumza kwa siri kuhusu Yesu. Wengine wakasema, “Huyu ni mtu mzuri.” Lakini wengine wakakataa na kusema, “Hapana, mtu huyo huwadanganya watu.” 13 Pamoja na hayo hakuwepo mtu aliyekuwa na busara zaidi kati yao kusema na Yesu kwa uwazi. Kwani waliwaogopa viongozi wa Wayahudi.

Yesu Afundisha Yerusalemu

14 Sherehe ile ilipokaribia kuisha, Yesu akaenda katika maeneo ya Hekalu na kuanza kufundisha. 15 Viongozi wa Kiyahudi waliomsikiliza walishangazwa na kusema, “Mtu huyu amejifunza wapi mambo haya yote? Yeye hakuwahi kupata mafundisho kama yale tuliyonayo.”

16 Yesu akajibu, “Ninayofundisha siyo yangu. Mafundisho yangu yanatoka kwake Yeye aliyenituma. 17 Watu wanaotaka kufanya kwa uhakika kama anavyotaka Mungu watafahamu kuwa mafundisho yangu yanatoka kwa Mungu. Watafahamu kwamba mafundisho haya siyo yangu. 18 Kama ningeyafundisha mawazo yangu, ningekuwa najitafutia heshima yangu mwenyewe. Lakini kama najaribu kumletea heshima Yeye aliyenituma, basi naweza kuaminiwa. Yeyote anayefanya kama hivyo hawezi kusema uongo. 19 Musa aliwapa sheria, sivyo? Lakini hamuitii hiyo sheria. Kama mnaitii, kwa nini basi mnataka kuniua?”

20 Watu wakamjibu Yesu, “Pepo amekuchanganya akili! Sisi hatuna mipango ya kukuua!”

21 Yesu akawambia, “Nilitenda ishara moja siku ya Sabato, na wote mkashangaa. 22 Lakini mnatii sheria aliyowapa Musa kuhusu kutahiriwa; nanyi mnatahiri hata siku ya Sabato! (Lakini hakika, Musa siye aliyewatahiri. Tohara Ilitoka kwa baba zenu walioishi kabla ya Musa.) Ndiyo, siku zote mnatahiri wana wenu hata siku ya Sabato. 23 Hii inaonesha kuwa mtu anaweza kutahiriwa siku ya Sabato ili kuitimiza sheria ya Musa. Sasa kwa nini mnanikasirikia mimi kwa kuuponya mwili wote wa mtu siku ya Sabato? 24 Acheni kuhukumu mambo ya watu kwa jinsi mnavyoyaona. Muwe makini kutoa kuhukumu kwa njia ya haki kabisa.”

Watu Wajiuliza Ikiwa Yesu Ni Masihi

25 Kisha baadhi ya watu waliokuwepo Yerusalemu wakasema, “Huyo ndiye mtu wanayetaka kumuua. 26 Lakini anafundisha mahali ambapo kila mtu anaweza kumwona na kumsikia. Wala hakuna anayejaribu kumzuia kufundisha. Inawezekana viongozi wamekubali kuwa kweli yeye ni Masihi. 27 Lakini Masihi halisi atakapokuja, hakuna atakayejua anakotoka. Nasi tunajua nyumbani kwake mtu huyu ni wapi.”

28 Yesu alikuwa bado anafundisha katika eneo la Hekalu aliposema kwa sauti, “Ni kweli mnanijua mimi na kule ninakotoka? Niko hapa, lakini siyo kwa matakwa yangu. Nilitumwa na Yeye aliye wa kweli. Lakini ninyi hamumjui. 29 Mimi namfahamu kwa sababu ninatoka kwake. Naye Ndiye aliyenituma.”

30 Yesu aliposema hivi, watu wakajaribu kumkamata. Lakini hakuna aliyethubutu hata kumgusa, kwa sababu wakati unaofaa kufanya hivyo ulikuwa bado haujafika. 31 Hata hivyo watu wengi wakamwamini Yesu. Wakasema, “Je, tunafikiri kuna haja ya kuendelea kumngojea Masihi mwingine aje atakayetenda ishara nyingine zaidi ya zile alizotenda mtu huyu?”

Viongozi wa Kiyahudi Wajaribu Kumkamata Yesu

32 Mafarisayo wakasikia yale ambayo watu walikuwa wakiyasema juu ya Yesu. Kwa sababu hiyo viongozi wa makuhani na Mafarisayo wakawatuma walinzi wa Hekalu kwenda kumkamata. 33 Kisha Yesu akasema, “Nitakuwa nanyi kwa muda mfupi. Kisha nitarudi kwake Yeye aliyenituma. 34 Ninyi mtanitafuta, lakini hamtaniona. Nanyi hamwezi kuja kule nitakapokuwa.”

35 Hawa Wayahudi wakaambiana wao kwa wao, “Huyu mtu atakwenda wapi sisi tusikoweza kufika? Je, anaweza kwenda kwenye miji ya Wayunani wanamoishi watu wetu? Je, atawafundisha Wayunani katika miji hiyo? 36 Anasema, ‘Mtanitafuta, lakini hamtaniona.’ Vile vile anasema, ‘Hamwezi kuja kule nitakapokwenda.’ Maana yake ni nini?”

Yesu Azungumza Juu ya Roho Mtakatifu

37 Siku ya mwisho ya kusherehekea sikukuu ikafika. Nayo Ilikuwa siku muhimu zaidi. Katika siku hiyo Yesu alisimama na kusema kwa sauti kubwa, “Yeyote aliye na kiu aje kwangu anywe. 38 Kama mtu ataniamini, mito ya maji yenye uzima itatiririka kutoka ndani ya moyo wake. Ndivyo Maandiko yanavyosema.” 39 Yesu alikuwa anazungumza juu ya Roho Mtakatifu ambaye alikuwa hajatolewa kwa watu bado, kwa sababu Yesu naye alikuwa bado hajatukuzwa. Ingawa baadaye, wale waliomwamini Yesu wangempokea huyo Roho.

Watu Wanabishana Juu ya Yesu

40 Watu waliposikia maneno aliyosema Yesu, baadhi yao wakasema, “Hakika mtu huyu ni nabii.”[a]

41 Wengine wakasema, “Huyu ni Masihi.”

Na wengine wakasema, “Masihi hawezi kutoka Galilaya. 42 Maandiko yanasema kwamba Masihi atatoka katika ukoo wa Daudi. Na wanasema kwamba atatoka Bethlehemu, mji alimoishi Daudi.” 43 Kwa jinsi hiyo watu hawakukubaliana wao kwa wao kuhusu Yesu. 44 Baadhi yao wakataka kumkamata. Lakini hakuna aliyejaribu kufanya hivyo.

Baadhi ya Viongozi wa Kiyahudi Wakataa Kuamini

45 Walinzi wa Hekalu wakarudi kwa viongozi wa makuhani na Mafarisayo. Makuhani na Mafarisayo wakawauliza, “Kwa nini hamjamleta Yesu?”

46 Walinzi wa Hekalu wakajibu, “Hatujawahi kumsikia mtu akisema mambo ya ajabu kiasi hicho!”

47 Mafarisayo wakajibu, “Kwa hiyo Yesu amewadanganya hata ninyi? 48 Hamuoni kuwa hakuna kiongozi yeyote wala sisi Mafarisayo anayemwamini? 49 Lakini watu hao walio nje wasiojua sheria wamo katika laana ya Mungu.”

50 Lakini Nikodemu alikuwa katika kundi lile. Naye ndiye yule aliyekwenda kumwona Yesu pale mwanzo.[b] Naye akasema, 51 “Sheria yetu haitaturuhusu kumhukumu mtu na kumtia hatiani kabla ya kumsikiliza kwanza na kuyaona aliyotenda?”

52 Viongozi wa Kiyahudi wakajibu, “Wewe nawe utakuwa umetoka Galilaya. Jifunze Maandiko. Hutapata lolote kuhusu nabii[c] anayetoka Galilaya.”

Mwanamke Afumaniwa Akizini

53 Kisha wote wakaondoka na kwenda nyumbani.

Footnotes

  1. 7:40 nabii Huenda walikuwa na maana nabii ambaye Mungu, alimwambia Musa ya kwamba atamtuma. Tazama Kum 18:15-19.
  2. 7:50 Naye ndiye … mwanzo Hadithi juu ya Nikodemo kwenda na kuongea na Yesu katika Yh 3:1-21.
  3. 7:52 kuhusu nabii Nakala mbili za kale za Kiyunani zina “Nabii”, ambayo ina maana “nabii kama vile Musa” anayetajwa katika Kum 18:15. Katika Mdo 3:22 na 7:37 hii inaeleweka kuwa ni Masihi kama katika mstari wa 40 hapo juu.

Jesus Goes to the Festival of Tabernacles

After this, Jesus went around in Galilee. He did not want[a] to go about in Judea because the Jewish leaders(A) there were looking for a way to kill him.(B) But when the Jewish Festival of Tabernacles(C) was near, Jesus’ brothers(D) said to him, “Leave Galilee and go to Judea, so that your disciples there may see the works you do. No one who wants to become a public figure acts in secret. Since you are doing these things, show yourself to the world.” For even his own brothers did not believe in him.(E)

Therefore Jesus told them, “My time(F) is not yet here; for you any time will do. The world cannot hate you, but it hates me(G) because I testify that its works are evil.(H) You go to the festival. I am not[b] going up to this festival, because my time(I) has not yet fully come.” After he had said this, he stayed in Galilee.

10 However, after his brothers had left for the festival, he went also, not publicly, but in secret. 11 Now at the festival the Jewish leaders were watching for Jesus(J) and asking, “Where is he?”

12 Among the crowds there was widespread whispering about him. Some said, “He is a good man.”

Others replied, “No, he deceives the people.”(K) 13 But no one would say anything publicly about him for fear of the leaders.(L)

Jesus Teaches at the Festival

14 Not until halfway through the festival did Jesus go up to the temple courts and begin to teach.(M) 15 The Jews(N) there were amazed and asked, “How did this man get such learning(O) without having been taught?”(P)

16 Jesus answered, “My teaching is not my own. It comes from the one who sent me.(Q) 17 Anyone who chooses to do the will of God will find out(R) whether my teaching comes from God or whether I speak on my own. 18 Whoever speaks on their own does so to gain personal glory,(S) but he who seeks the glory of the one who sent him is a man of truth; there is nothing false about him. 19 Has not Moses given you the law?(T) Yet not one of you keeps the law. Why are you trying to kill me?”(U)

20 “You are demon-possessed,”(V) the crowd answered. “Who is trying to kill you?”

21 Jesus said to them, “I did one miracle,(W) and you are all amazed. 22 Yet, because Moses gave you circumcision(X) (though actually it did not come from Moses, but from the patriarchs),(Y) you circumcise a boy on the Sabbath. 23 Now if a boy can be circumcised on the Sabbath so that the law of Moses may not be broken, why are you angry with me for healing a man’s whole body on the Sabbath? 24 Stop judging by mere appearances, but instead judge correctly.”(Z)

Division Over Who Jesus Is

25 At that point some of the people of Jerusalem began to ask, “Isn’t this the man they are trying to kill?(AA) 26 Here he is, speaking publicly, and they are not saying a word to him. Have the authorities(AB) really concluded that he is the Messiah?(AC) 27 But we know where this man is from;(AD) when the Messiah comes, no one will know where he is from.”

28 Then Jesus, still teaching in the temple courts,(AE) cried out, “Yes, you know me, and you know where I am from.(AF) I am not here on my own authority, but he who sent me is true.(AG) You do not know him, 29 but I know him(AH) because I am from him and he sent me.”(AI)

30 At this they tried to seize him, but no one laid a hand on him,(AJ) because his hour had not yet come.(AK) 31 Still, many in the crowd believed in him.(AL) They said, “When the Messiah comes, will he perform more signs(AM) than this man?”

32 The Pharisees heard the crowd whispering such things about him. Then the chief priests and the Pharisees sent temple guards to arrest him.

33 Jesus said, “I am with you for only a short time,(AN) and then I am going to the one who sent me.(AO) 34 You will look for me, but you will not find me; and where I am, you cannot come.”(AP)

35 The Jews said to one another, “Where does this man intend to go that we cannot find him? Will he go where our people live scattered(AQ) among the Greeks,(AR) and teach the Greeks? 36 What did he mean when he said, ‘You will look for me, but you will not find me,’ and ‘Where I am, you cannot come’?”(AS)

37 On the last and greatest day of the festival,(AT) Jesus stood and said in a loud voice, “Let anyone who is thirsty come to me and drink.(AU) 38 Whoever believes(AV) in me, as Scripture has said,(AW) rivers of living water(AX) will flow from within them.”[c](AY) 39 By this he meant the Spirit,(AZ) whom those who believed in him were later to receive.(BA) Up to that time the Spirit had not been given, since Jesus had not yet been glorified.(BB)

40 On hearing his words, some of the people said, “Surely this man is the Prophet.”(BC)

41 Others said, “He is the Messiah.”

Still others asked, “How can the Messiah come from Galilee?(BD) 42 Does not Scripture say that the Messiah will come from David’s descendants(BE) and from Bethlehem,(BF) the town where David lived?” 43 Thus the people were divided(BG) because of Jesus. 44 Some wanted to seize him, but no one laid a hand on him.(BH)

Unbelief of the Jewish Leaders

45 Finally the temple guards went back to the chief priests and the Pharisees, who asked them, “Why didn’t you bring him in?”

46 “No one ever spoke the way this man does,”(BI) the guards replied.

47 “You mean he has deceived you also?”(BJ) the Pharisees retorted. 48 “Have any of the rulers or of the Pharisees believed in him?(BK) 49 No! But this mob that knows nothing of the law—there is a curse on them.”

50 Nicodemus,(BL) who had gone to Jesus earlier and who was one of their own number, asked, 51 “Does our law condemn a man without first hearing him to find out what he has been doing?”

52 They replied, “Are you from Galilee, too? Look into it, and you will find that a prophet does not come out of Galilee.”(BM)


[The earliest manuscripts and many other ancient witnesses do not have John 7:53—8:11. A few manuscripts include these verses, wholly or in part, after John 7:36, John 21:25, Luke 21:38 or Luke 24:53.]

53 Then they all went home,

Footnotes

  1. John 7:1 Some manuscripts not have authority
  2. John 7:8 Some manuscripts not yet
  3. John 7:38 Or me. And let anyone drink 38 who believes in me.” As Scripture has said, “Out of him (or them) will flow rivers of living water.”