Add parallel Print Page Options

29 Mara baada ya mateso ya siku hizo, mambo haya yatatokea:

‘Jua litakuwa jeusi,
    na mwezi hautatoa mwanga.
Nyota zitaanguka kutoka angani,
    na kila kitu kilicho angani
    kitatikiswa kutoka mahali pake.’[a]

30 Kisha kutatokea ishara angani kuwa Mwana wa Adamu anakuja. Watu wote wa ulimwengu watajipiga kifuani wakiomboleza. Kila mtu atamwona Mwana wa Adamu akija katika mawingu ya angani akiwa na nguvu na utukufu mkuu. 31 Naye atatumia parapanda kuu kuwatuma malaika zake kila mahali duniani. Nao watawakusanya wateule wake kutoka mwisho mmoja wa mbingu hadi mwingine.

Read full chapter

Footnotes

  1. 24:29 Tazama Isa 13:10; 34:4.