Petro Aeleza Alivyotumwa Kwa Mataifa

11 Baadaye mitume na waamini wa sehemu zote za Yudea wakapata habari kwamba watu wasiokuwa Wayahudi nao wamepokea neno la Mungu. Kwa hiyo Petro alipokwenda Yerusalemu, wale waliokuwa wakishikilia sheria ya tohara walimshutumu wakasema, “Kwa nini ulikwenda kwa watu wasiotahiriwa na kula pamoja nao?” Ndipo Petro akaanza kuwaeleza mambo yote yalivyotokea akasema, “Nil ikuwa nikiomba katika mji wa Jopa, nikaona katika ndoto kitu kama shuka kubwa ikishushwa chini kwa ncha zake nne, kutoka mbinguni, nayo ikanifikia. Nilipotazama kwa makini nikaona wanyama wa kila aina, wanyama wa mwituni, wanyama watambaao na ndege wa angani. Nikasikia sauti ikiniambia, ‘Amka Petro, chinja, ule!’ Nami nikasema, ‘La, Bwana! Sijawahi kula kitu cho chote kili chokatazwa na sheria zetu.’ Lakini ile sauti kutoka mbinguni ikasema kwa mara ya pili, ‘Usiite kitu cho chote alichokitakasa Mungu kuwa ni uchafu.’ 10 Jambo hili lilitokea mara tatu ndipo vyote vikachukuliwa tena mpaka mbinguni. 11 Wakati huo huo watu watatu waliokuwa wametumwa kutoka Kaisaria wakawasili katika nyumba niliyokuwa nikikaa. 12 Roho akaniambia niende nao bila kusita. Nikaenda nao nikisindikizwa na hawa ndugu sita, tukaingia katika nyumba ya Kornelio. 13 Kornelio akatuambia jinsi malaika alivyomtokea akamwambia, ‘Tuma watu Jopa wakamwite Simoni aitwaye Petro. 14 Yeye anao ujumbe utakaokuokoa wewe na wote walio nyum bani mwako.’ 15 Nami nilipokuwa nikisema nao, Roho Mtakatifu akashuka juu yao kama alivyotushukia sisi mwanzoni. 16 Nami nikakumbuka jinsi Bwana alivyosema, ‘Yohana alibatiza kwa maji, lakini ninyi mtabatizwa kwa Roho Mtakatifu.’ 17 Basi kwa kuwa Mungu ndiye aliyewapa hawa watu karama ile ile aliyotupa sisi tulipomwamini Bwana Yesu, mimi ni nani hata nimpinge Mungu?” 18 Nao waliposikia maneno haya hawakuwa na la kusema. Wakamsifu Mungu, wakasema, “Mungu amewapa watu wa mataifa nafasi ya kutubu na kupokea uzima wa milele.’ ’

Kanisa Laenea Antiokia

19 Wale waamini waliotawanyika kutoka Yerusalemu wakati wa mateso yaliyotokana na kifo cha Stefano, walisafiri hadi Foinike na Kipro na Antiokia. Wakawa wakihubiri Habari Njema kwa Wayahudi peke yake. 20 Lakini baadhi yao walikwenda Antiokia wakitokea Kipro na Kirene. Wakawaambia Wagiriki Habari Njema za Bwana Yesu. 21 Roho wa Bwana alikuwa pamoja nao kwa hiyo watu wengi wakaamini na kumgeukia Bwana. 22 Habari hizi zilipowafikia vion gozi wa kanisa huko Yerusalemu, walimtuma Barnaba aende Antiokia. 23 Alipofika akaona jinsi Mungu alivyokuwa akiwabariki watu kwa neema yake, alifurahi sana akawatia moyo waendelee kwa juhudi kuwa waaminifu kwa Bwana. 24 Barnaba alikuwa mtu mwema aliyejawa Roho Mtakatifu, mwenye imani kuu; na watu wengi waliongoka wakam wamini Bwana. 25 Kisha Barnaba akasafiri kwenda Tarso kumtafuta Sauli. 26 Alipompata akaja naye mpaka Antiokia. Na wote wawili wakakaa huko kwa mwaka mzima, wakiwafundisha wengi walioamini katika kanisa la Antiokia. Hapo Antiokia ndipo waamini waliitwa ‘Wakristo’ kwa mara ya kwanza.

27 Wakati huu manabii walitoka Yerusalemu wakaenda Antiokia. 28 Na mmoja wao, jina lake Agabo, akasimama katika mkutano aka tabiri kwa uweza wa Roho kwamba pangetokea njaa kubwa dunia nzima. Njaa hiyo ilitokea wakati Klaudio alipokuwa mtawala. 29 Waamini wakaamua kwamba kila mtu, kulingana na uwezo alio nao, atoe msaada upelekwe kwa ndugu waliokuwa wanaishi Yudea. 30 Wakafanya hivyo, na misaada ikapelekwa na Barnaba na Sauli kwa wazee wa kanisa.