Yesu Ajaribiwa Na Shetani

Kisha Yesu akaongozwa na Roho Mtakatifu mpaka nyikani ili akajaribiwe na shetani. Akakaa huko siku arobaini akifunga, pasipo kula kitu cho chote mchana na usiku, hatimaye akaona njaa. Ndipo shetani akamjia akamwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, amuru mawe haya yawe mikate.”

Mungu, amuru mawe haya yawe mikate.”

Lakini Yesu akamjibu, “Imeandikwa, ‘Mtu hataishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno analotamka Mungu.’ ”

Ndipo shetani akampeleka Yesu mpaka mji mtakatifu wa Yerus alemu, akamweka juu ya mnara wa Hekalu, akamwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu jitupe chini; kwa kuwa imeandikwa, ‘Atawaagiza malaika wake wakuhudumie,’ na, ‘Watakuinua juu mikononi mwao ili usijikwae mguu wako kwenye jiwe.’ ”

Yesu akamjibu, “Pia imeandikwa, ‘Usimjaribu Bwana Mungu wako.’ ”

Kwa mara nyingine shetani akamchukua Yesu mpaka kwenye kilele cha mlima mrefu akamwonyesha milki zote za dunia na fahari zake, kisha akamwambia, “Nitakupa hivi vyote kama ukipiga magoti na kuniabudu.”

10 Yesu akamwambia, “Ondoka hapa shetani! Kwa maana imean dikwa, ‘Utamwabudu Bwana Mungu wako na utamtumikia yeye peke yake.’ ” 11 Ndipo shetani akamwacha, na malaika wakaja wakamhu dumia.

Yesu Aanza Kuhubiri

12 Yesu aliposikia kwamba Yohana Mbatizaji alikuwa ameka matwa na kuwekwa gerezani, alirudi Galilaya. 13 Akaondoka Nazareti akaenda kuishi Kapernaumu karibu na ziwa, katika eneo la Zabuloni na Naftali. 14 Utabiri wa nabii Isaya ukatimia, kama alivyosema: 15 “Nchi ya Zabuloni na nchi ya Naftali, kuelekea baharini, ng’ambo ya Yordani, Galilaya ya watu wa mataifa - 16 watu wale waishio katika giza wameona nuru kuu; na kwa wale wanaoishi katika nchi ya giza la mauti, nuru imewaangazia.” 17 Tangu wakati huo, Yesu alianza kuhubiri akisema: “Tubuni, kwa maana Ufalme wa mbinguni umekaribia.”

Yesu Awaita Wanafunzi Wanne

18 Yesu alipokuwa akitembea kando kando ya ziwa la Galilaya aliwaona ndugu wawili, Simoni ambaye aliitwa Petro na Andrea ndugu yake. Walikuwa katika mashua wakitupa nyavu zao baharini kwa maana wao walikuwa wavuvi.

19 Yesu akawaambia, “Nifuateni, nami nitawafanya muwe wavuvi wa watu.” 20 Wakaziacha nyavu zao mara moja, wakamfuata.

21 Alipoendelea mbele kidogo, aliwakuta ndugu wengine wawili, Yakobo na Yohana, wakiwa wamekaa kwenye mashua pamoja na baba yao Zebedayo wakishona nyavu zao; akawaita. 22 Wakaacha nyavu zao mara moja, wakamfuata.

Yesu Ahubiri Na Kuponya Wagonjwa

23 Yesu alizunguka Galilaya yote, akifundisha katika masi nagogi na kuhubiri Habari Njema ya Ufalme wa mbinguni, na kupo nya kila ugonjwa na kila udhaifu. 24 Kwa hiyo sifa zake zilienea sehemu zote za Siria. Nao wakamletea wagonjwa wote, waliosumbu liwa na maradhi mbalimbali na maumivu, watu waliopagawa na mashe tani, wenye kifafa na waliopooza, naye akawaponya.

25 Umati mkubwa wa watu ukamfuata kutoka Galilaya, Dekapoli, Yerusalemu, Yudea na kutoka ng’ambo ya mto Yordani.