Dalili Za Siku Za Mwisho

24 Yesu aliondoka Hekaluni na alipokuwa akienda zake, wana funzi wakamwendea ili wakamwonyeshe majengo ya Hekalu. Lakini yeye akawaambia, “Mnayaona haya yote? Nawaambieni kweli, hakuna hata jiwe moja hapa litakalobaki juu ya jingine, yote yatatupwa chini.”

Yesu alipokuwa ameketi kwenye mlima wa Mizeituni wanafunzi wake walimwendea faraghani, wakamwuliza, “Tueleze, mambo haya yatatokea lini na ni dalili gani zitaonyesha kuja kwako na mwisho wa dunia?”

Yesu akawajibu, “Jihadharini, mtu asije akawadanganya. Kwa maana wengi watakuja kwa jina langu wakisema, ‘Mimi ndiye Kristo’ nao watawapotosha wengi. Mtasikia habari za vita na tetesi za vita, msitishike; kwa maana haya hayana budi kutokea; lakini mwisho utakuwa bado. Taifa kwa taifa na nchi kwa nchi zitapigana. Kutakuwa na njaa na tetemeko la ardhi sehemu mbalim bali. Haya yote yatakuwa kama mwanzo wa uchungu wa uzazi.

“Kisha mtasalitiwa, mtateswa na kuuawa na mtachukiwa na watu wa mataifa yote kwa ajili ya jina langu. 10 Wakati huo, wengi wataacha imani yao, watasalitiana na kuchukiana, 11 na watatokea manabii wengi wa uongo ambao watawapotosha watu. 12 Kwa sababu uovu utakuwa umeenea sana, upendo wa watu wengi utapoa. 13 Lakini mtu atakayesimama imara mpaka mwisho, ataoko lewa. 14 Na hii Habari Njema ya Ufalme itahubiriwa ulimwenguni pote, kama ushuhuda kwa mataifa yote. Ndipo mwisho utafika.

15 “Mtakapoona lile ‘Chukizo la Uharibifu’ linalozungumzwa na nabii Danieli limesimama mahali Patakatifu - msomaji na aelewe - 16 basi wale walioko Yudea wakimbilie milimani. 17 Aliyeko juu ya nyumba asishuke kuchukua vitu vyake ndani. 18 Aliyeko sham bani asirudi nyumbani kuchukua vazi lake. 19 Ole wao wanawake watakaokuwa na mimba na watakaokuwa wakinyonyesha siku hizo! 20 Ombeni ili mtakapokuwa mnakimbia, isiwe ni kipindi cha baridi au siku ya sabato. 21 Kwa maana kutakuwa na dhiki kuu ambayo haijawahi kutokea tangu mwanzo wa dunia mpaka sasa na ambayo haitatokea tena. 22 Kama siku hizo zisingepunguzwa, hakuna hata mtu mmoja ambaye angesalimika, lakini kwa ajili ya wale walioteu liwa na Mungu, siku hizo zitapunguzwa. 23 Wakati huo mtu aki waambia, ‘Tazama! Kristo yuko hapa!’ au ‘Kristo yule pale!’ msi sadiki. 24 Kwa maana watatokea makristo na manabii wa uongo na watafanya ishara za ajabu na miujiza mingi ili kuwadanganya, hata ikiwezekana, wateule wa Mungu. 25 Angalieni, nawatahadharisha mapema.

26 “Kwa hiyo wakiwaambia, ‘Yule kule nyikani,’ msitoke. Au wakisema, ‘Yuko chumbani 27 Kwa maana kama vile umeme unavyotokea mashariki na kuangaza mpaka magharibi, ndivyo itakavyokuwa kuja kwangu mimi Mwana wa Adamu. 28 Kwa maana po pote ulipo mzoga, ndipo wakusanyikapo tai.

29 “Mara baada ya dhiki ya wakati huo, jua litatiwa giza, mwezi hautatoa mwanga wake tena, na nyota zitaanguka kutoka mbin guni; nguvu za anga zitatikisika. 30 Ndipo itaonekana ishara ya Mwana wa Adamu angani na watu wote ulimwenguni wataomboleza. Nao wataniona mimi Mwana wa Adamu nikija juu ya mawingu ya angani, katika uwezo na utukufu mkuu. 31 Na nitawatuma malaika zangu kwa sauti kuu ya tarumbeta na watawakusanya wateule wangu kutoka pande zote nne za dunia, kutoka mwisho mmoja wa mbingu hadi mwisho mwingine.

32 “Jifunzeni kutoka kwa mti wa mtini. Matawi yake yana poanza kuwa laini na majani kuchipua, mnafahamu kwamba kiangazi kimekaribia. 33 Basi, pia mkiona dalili hizi, fahamuni kwamba amekaribia kurudi, na yu karibu na mlango. 34 Nawaambieni kweli, hakika kizazi hiki hakitapita kabla mambo haya hayajatokea. 35 Mbingu na dunia zitatoweka, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.”

Hakuna Ajuaye Siku Wala Saa

36 “Hakuna ajuaye siku wala saa, hata malaika mbinguni wala Mwana, isipokuwa Baba peke yake. 37 Kama ilivyokuwa wakati wa Nuhu, ndivyo itakavyokuwa atakaporudi Mwana wa Adamu. 38 Kwa maana siku zile kabla ya gharika, watu walikuwa wakila na kunywa, wakioa na kuolewa, mpaka siku ile Nuhu alipoingia kwenye safina. 39 Nao hawakujua ni nini kitatokea mpaka gharika ilipokuja ika wakumba wote. Hivyo ndivyo itakavyokuwa nitakapokuja mimi Mwana wa Adamu.

40 “Watu wawili watakuwa shambani; mmoja atachukuliwa, mwingine ataachwa. 41 Wanawake wawili watakuwa wanatwanga; mmoja atachukuliwa, mwingine ataachwa.

42 “Kwa hiyo kesheni, kwa maana hamjui ni siku gani ataka pokuja Bwana wenu.

43 “Lakini fahamuni kwamba, kama mwenye nyumba angalifahamu ni saa ngapi za usiku ambapo mwizi atakuja, angalikaa macho asiache nyumba yake ivunjwe. 44 Kwa hiyo ninyi pia lazima muwe tayari kwa maana mimi Mwana wa Adamu nitakuja saa ambayo hamnita zamii.”

Mfano Wa Mtumishi Mwaminifu

45 “Basi, ni nani mtumishi mwaminifu ambaye bwana wake amemweka awe msimamizi wa watumishi wengine nyumbani kwake, awape posho yao kwa wakati wake? 46 Heri mtumishi ambaye atakapokuja bwana wake atamkuta anafanya hivyo. 47 Nawaambieni kweli, atam fanya mtumishi huyo asimamie mali yake yote.

48 “Lakini kama mtumishi huyo ni mwovu atasema moyoni mwake, ‘Bwana wangu hatarudi kwa muda mrefu,’ 49 na ataanza kuwapiga watumishi wenzake na kula na kunywa na walevi. 50 Bwana wake atakuja wakati ambapo mtumishi huyo hamtazamii na saa ambayo haijui. 51 Ndipo atamwadhibu huyo mtumishi na kumweka katika kundi la wanafiki; huko kutakuwa na kilio na kusaga meno.”

Yesu Aonya Kuhusu Wakati Ujao

(Mk 13:1-31; Lk 21:5-33)

24 Yesu alipokuwa anaondoka eneo la Hekalu, wanafunzi wake walimwendea na kumwonyesha majengo ya Hekalu. Akawauliza, “Mnayaona majengo haya? Ukweli ni kuwa, yataharibiwa. Kila jiwe litadondoshwa chini, hakuna jiwe litakaloachwa juu ya jiwe jingine.”

Baadaye, Yesu alipokuwa ameketi mahali fulani katika Mlima wa Mizeituni, Wafuasi wake walimwendea faraghani. Wakasema, “Twambie mambo haya yatatokea lini. Na nini kitatokea ili kutuandaa kwa ajili ya ujio wako na mwisho wa nyakati?”

Yesu akajibu, “Mjihadhari! Msimruhusu mtu yeyote awadanganye. Watu wengi watakuja na watatumia jina langu. Watasema, ‘Mimi ndiye Masihi.’ Na watawadanganya watu wengi. Mtasikia kuhusu vita vinanavyopiganwa na pia matetesi ya kuwapo vita vingine. Lakini msiogope. Mambo haya lazima yatokee na mwisho wenyewe hautafuata palepale. Mataifa yatapigana na mataifa mengine. Falme zitapigana na falme zingine. Utakuwepo wakati wa njaa ambapo watu watakosa chakula. Na kutakuwa matetemeko ya ardhi sehemu mbalimbali. Mambo haya ni mwanzo wa matatizo, kama uchungu wa kwanza mwanamke anapozaa.

Kisha mtakamatwa na kupelekwa kwa wenye mamlaka ili mhukumiwe na kuuawa. Watu wote katika ulimwengu watawachukia kwa sababu mnaniamini mimi. 10 Nyakati hizo watu wengi wataacha kuwa wafuasi wangu. Watasalitiana na kuchukiana. 11 Manabii wengi watatokea na kusababisha watu wengi kuamini mambo yasiyo ya kweli. 12 Kutakuwepo na uovu mwingi sana duniani kiasi kwamba upendo wa waaminio wengi utapoa. 13 Lakini yeyote yule atakayekuwa mwaminifu mpaka mwisho ataokolewa. 14 Na Habari Njema niliyoihubiri kuhusu Ufalme wa Mungu itahubiriwa ulimwenguni kote. Itatawanywa katika kila taifa. Kisha mwisho utakuja.

15 Nabii Danieli alizungumza kuhusu ‘jambo la kutisha litakalosababisha uharibifu.’[a] Mtakapoliona jambo hili la kutisha limesimama patakatifu.” (Asomaye hili anapaswa kuelewa jambo hili linamaanisha nini.) 16 “Watu walio Uyahudi wakimbilie milimani. 17 Wakimbie pasipo kupoteza muda ili kuchukua kitu chochote. Wakiwa darini wasiteremke ili kuchukua kitu na kukitoa nje ya nyumba. 18 Wakiwa shambani wasirudi nyumbani kuchukua koti.

19 Itakuwa hali ngumu kwa wanawake wenye mimba na wenye watoto wachanga! 20 Ombeni isiwe majira ya baridi au isiwe siku ya Sabato mambo haya yatakapotokea na mkalazimika kukimbia, 21 kwa sababu utakuwa wakati wa dhiki kuu. Kutakuwepo na usumbufu mwingi sana kuliko ule uliowahi kutokea tangu mwanzo wa ulimwengu. Na hakuna jambo baya kama hilo litakalotokea tena.

22 Lakini Mungu amekwisha amua kuufupisha wakati huo. Ikiwa usingefupishwa, hakuna ambaye angeendelea kuishi. Lakini Mungu ataufupisha ili kuwasaidia watu aliowachagua.

23 Wakati huo watu wataweza kuwaambia, ‘Tazama, Masihi yuko kule!’ Au wakasema, ‘Ni yule!’ Msiwaamini. 24 Manabii wa uongo na masihi wa uongo watatokea na kufanya miujiza na maajabu[b] makuu, ili ikiwezekana wawadanganye wateule. 25 Na sasa nimewatahadharisha kuhusu hili kabla halijatokea.

Yesu Atakaporudi Tena

(Mk 13:24-31; Lk 17:23-24,37; 21:25-32)

26 Inawezekana mtaambiwa, ‘Masihi yuko jangwani!’ Msiende jangwani kumtafuta. Mtu mwingine anaweza akasema, ‘Masihi yuko katika chumba kile!’ Msiamini. 27 Mwana wa Adamu atakapokuja, kila mtu atamwona. Itakuwa kama radi inavyowaka angani na kuonekana kila mahali. 28 Ni kama kutafuta mzoga: Mzoga hupatikana mahali ambapo tai wengi wamekusanyika.

29 Mara baada ya mateso ya siku hizo, mambo haya yatatokea:

‘Jua litakuwa jeusi,
    na mwezi hautatoa mwanga.
Nyota zitaanguka kutoka angani,
    na kila kitu kilicho angani
    kitatikiswa kutoka mahali pake.’[c]

30 Kisha kutatokea ishara angani kuwa Mwana wa Adamu anakuja. Watu wote wa ulimwengu watajipiga kifuani wakiomboleza. Kila mtu atamwona Mwana wa Adamu akija katika mawingu ya angani akiwa na nguvu na utukufu mkuu. 31 Naye atatumia parapanda kuu kuwatuma malaika zake kila mahali duniani. Nao watawakusanya wateule wake kutoka mwisho mmoja wa mbingu hadi mwingine.

32 Jifunze kwa mtini: Matawi yake yanapokuwa ya kijani na laini na kuanza kutoa majani mapya, ndipo mnatambua kuwa majira ya joto yamekaribia. 33 Katika namna hiyo hiyo, mtakapoona mambo haya yote yakitokea, mtajua kuwa wakati[d] umekaribia wa kile kitakachotokea. 34 Ninawahakikishia kuwa mambo haya yote yatatokea wakati ambao baadhi ya watu wa nyakati hizi wakiwa bado hai. 35 Ulimwengu wote, dunia na anga vitaangamizwa, lakini maneno yangu yatadumu milele.

Mungu Peke Yake Ndiye Ajuaye Siku ya Kurudi kwa Mwana wa Adamu

(Mk 13:32,35; Lk 17:26-30,34-36)

36 Hakuna anayeijua siku wala wakati. Malaika wa mbinguni hawaijui hata Mwana hajui itakuwa lini. Baba peke yake ndiye anayejua.

37 Mwana wa Adamu atakapokuja, itakuwa kama ilivyokuwa nyakati za Nuhu. 38 Siku zile kabla ya gharika, watu walikuwa wakila na kunywa, wakioa na kuwatoa binti zao kuolewa mpaka siku ambayo Nuhu aliingia kwenye safina. 39 Hawakujua juu ya kilichokuwa kinaendelea mpaka mafuriko yalipowajia na kuwaangamiza wote.

Ndiyo itakavyokuwa Mwana wa Adamu atakapokuja. 40 Wanaume wawili watakuwa wakifanya kazi shambani, mmoja atachukuliwa na mwingine ataachwa. 41 Wanawake wawili watakuwa wanasaga nafaka pamoja, mmoja atachukuliwa na mwingine ataachwa.

42 Hivyo iweni tayari daima. Hamjui siku ambayo Bwana wenu atarudi. 43 Mwenye nyumba angefanya nini ikiwa angejua wakati ambao mwizi atakuja? Mnajua angelikesha ili mwizi asivunje na kuingia. 44 Hivyo, ninyi nanyi iweni tayari. Mwana wa Adamu atakuja katika wakati msiomtarajia.

Watumishi Wema na Wabaya

(Mk 13:33-37; Lk 12:41-48)

45 Fikiria mtumishi aliyewekwa na bwana wake kuwapa chakula watumishi wake wengine katika muda uliopangwa. Ni kwa namna gani mtumishi huyo atajionyesha kuwa ni mwangalifu na mwaminifu? 46 Bwana wake atakaporudi na kumkuta anafanya kazi aliyompa, siku hiyo itakuwa siku ya furaha kwa mtumishi huyo. 47 Ninawaambia bila mashaka yoyote kuwa, bwana wake atamchagua mtumishi huyo awe msimamizi wa kila kitu anachomiliki yule Bwana.

48 Lakini nini kitatokea ikiwa mtumishi huyo ni mbaya na akadhani kuwa bwana wake hatarudi karibuni? 49 Ataanza kuwapiga watumishi wengine na kuanza kunywa na kula na walevi. 50 Ndipo bwana wake atakuja wakati asioutarajia, ambapo mtumishi hakujiandaa. 51 Bwana atamwadhibu mtumishi huyo na kumpeleka anakostahili kuwapo pamoja na watumishi wengine waliojifanya kuwa wema. Huko watalia na kusaga meno kwa maumivu.

Footnotes

  1. 24:15 jambo … uharibifu Tazama Dan 9:27; 12:11 (pia Dan 11:31).
  2. 24:24 miujiza na maajabu Hapa ina maana ya kazi za ajabu zinazofanywa kwa kutumia nguvu za Shetani.
  3. 24:29 Tazama Isa 13:10; 34:4.
  4. 24:33 wakati Wakati ambao Yesu aliuzungumzia ni ule ambapo kitu muhimu kitatokea. Tazama Lk 21:31, pale ambapo Yesu anasema huu ni wakati wa Ufalme wa Mungu kutufikia.