Add parallel Print Page Options

Nani ni Mkuu Zaidi?

(Mt 18:1-5; Lk 9:46-48)

33 Kisha wakaja Kapernaumu. Na Yesu alipokuwa ndani ya nyumba aliwauliza, “Je, mlikuwa mnajidiliana nini njiani?” 34 Lakini wao walinyamaza kimya, kwa sababu njiani walikuwa wamebishana juu ya nani kati yao alikuwa ni mkuu zaidi.

35 Hivyo Yesu aliketi chini, akawaita wale kumi na mbili, na akawaambia, “Ikiwa yupo mtu yeyote anayetaka kuwa wa kwanza, inapasa basi awe wa mwisho kuliko wote na mtumishi wa wote.”

36 Akamchukua mtoto mdogo mikononi mwake na kumsimamisha mbele yao. Akimkumbatia mtoto huyo, Yesu alisema, 37 “Yeyote atakayemkaribisha mtoto mdogo kama huyu hapa kwa sababu ya jina langu basi ananikaribisha na mimi pia. Yeyote anayenikubali mimi hanikubali mimi tu bali anamkubali pia yeye aliyenituma.”

Read full chapter

Mabishano Kuhusu Aliye Mkuu

33 Basi wakafika Kapernaumu na baada ya kuingia nyumbani akawauliza, “Mlikuwa mnabishana nini njiani?” 34 Lakini hawa kumjibu, kwa sababu njiani walikuwa wakibishana kuhusu nani kati yao alikuwa mkuu zaidi.

35 Akaketi chini, akawaita wote kumi na wawili akawaambia: “Mtu anayetaka kuwa kiongozi hana budi kuwa wa chini kuliko wote na kuwa mtumishi wa wote.” 36 Kisha akamchukua mtoto mdogo akamweka mbele yao, akamkumbatia akawaambia, 37 “Mtu ye yote amkaribishaye mmoja wa hawa watoto wadogo, ananikaribisha mimi. Na ye yote anayenikaribisha mimi anamkaribisha Baba yangu ali yenituma.”

Read full chapter