Add parallel Print Page Options

Petro Atambua Yesu ni Nani

(Mt 16:13-19; Mk 8:27-29)

18 Wakati mmoja Yesu alikuwa anaomba akiwa peke yake. Wafuasi wake walimwendea na aliwauliza, “Watu wanasema mimi ni nani?”

19 Wakajibu, “Baadhi ya watu wanasema wewe ni Yohana Mbatizaji, wengine wanasema wewe ni Eliya, lakini wengine wanasema wewe ni mmoja wa manabii wa zamani aliyefufuka.”

20 Kisha Yesu akawauliza wafuasi wake, “Na ninyi mnasema mimi ni nani?”

Petro akajibu, “Wewe ni Masihi kutoka kwa Mungu.”

21 Yesu akawatahadharisha wasimwambie mtu yeyote.

Read full chapter