Font Size
Luka 6:12-16
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Luka 6:12-16
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Yesu Achagua Wanafunzi Wake Kumi na Wawili
(Mt 10:1-4; Mk 3:13-19)
12 Siku chache baadaye, Yesu alikwenda mlimani kuomba. Alikaa huko usiku kucha akimwomba Mungu. 13 Asubuhi iliyofuata aliwaita wafuasi wake, akachagua kumi na wawili miongoni mwao na kuwaita Mitume. Nao ni:
14 Simoni (ambaye Yesu alimwita Petro),
Andrea aliyekuwa kaka yake Petro,
Yakobo,
Yohana,
Filipo,
Bartholomayo,
15 Mathayo na
Tomaso,
Yakobo mwana wa Alfayo,
Simoni aliyeitwa Mzelote,
16 Yuda mwana wa Yakobo,
na Yuda Iskariote (yule ambaye baadaye alimsaliti Yesu).
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)
Copyright © 2017 by Bible League International