Yesu Ajaribiwa Na Shetani

Kisha Yesu, akiwa amejaa Roho Mtakatifu, akarudi kutoka Yordani akaongozwa hadi jangwani. Alikaa huko jangwani siku arobaini akijaribiwa na shetani. Siku zote hizo hakula cho chote , kwa hiyo baada ya muda huo aliona njaa.

Shetani akamwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, amuru jiwe hili liwe mkate.”

Yesu akamjibu, “Imeandikwa katika maandiko, ‘mtu haishi kwa chakula tu.’ ”

Kisha shetani akamchukua hadi juu ya mlima mrefu akamwo nyesha kwa mara moja milki zote za dunia. 6-7 Akamwambia, “Uki piga magoti na kuniabudu, nitakupa uwezo juu ya milki zote hizi na fahari yake; maana ni zangu na ninaweza kumpa ye yote nita kaye.” Yesu akamjibu, “Imeandikwa: ‘Mwabudu Bwana Mungu wako na kumtumikia yeye peke yake.’ ”

9-11 Ndipo shetani akamfikisha Yerusalemu, akampand isha juu ya mnara wa Hekalu, akamwambia: “Kama wewe ndiwe Mwana wa Mungu, jitupe chini kwani imeandikwa, ‘Mungu ataamrisha mal aika wake wakulinde

12 Yesu akamwambia, “Pia imeandikwa, ‘Usimjaribu Bwana Mungu wako.’ ”

Mungu wako.’ ”

13 Basi Shetani alipomaliza majaribu yote, akamwacha Yesu kwa muda.

Yesu Ahubiri Galilaya

14 Kisha Yesu akarudi Galilaya, akiwa amejaa nguvu za Roho Mtakatifu. Habari zake zikaenea katika sehemu zote za wilaya ile. 15 Alifundisha katika masinagogi yao na wote wakamsifu.

Yesu Akataliwa Na Watu Wa Nazareti

16 Baadaye Yesu akaenda Nazareti, mahali alipokulia. Siku ya sabato alikwenda katika sinagogi kama kawaida yake. Akasimama ili asome Maandiko. 17 Akapewa kitabu cha nabii Isaya, akakifun gua mahali palipoandikwa: 18-19 “Roho wa Bwana yu juu yangu. Amenichagua kuwahubiria maskini Habari Njema. Amenituma kuwatan gazia wafungwa kuwa wako huru, kuwaambia vipofu kuwa wanaweza kuona tena; na kuwaweka huru wanaoonewa, na nitangaze mwaka ambao Bwana atawabariki watu wake.” 20 Akakifunga kitabu, akamrud ishia mtumishi, akaketi; na watu wote waliokuwamo katika sinagogi wakamkazia macho. 21 Ndipo akasema: “Maandiko haya mliyosikia nikisoma, leo yametimia.”

22 Wote waliokuwako wakamsifu na kuyastaajabia maneno yake mazuri, wakaulizana, “Je, huyu si yule mtoto wa Yusufu?” 23 Lakini akawajibu, “Bila shaka mtaniambia, ‘Daktari, jiponye! Mbona hutendi hapa kijijini kwako miujiza tuliyosikia kuwa umeifanya kule Kapernaumu?’ 24 Ningependa mfahamu ya kwamba hakuna nabii anayekubaliwa na watu kijijini kwake. 25 Nawahakik ishieni kwamba walikuwepo wajane wengi katika Israeli wakati wa Eliya, mvua ilipoacha kunyesha kwa miaka mitatu na nusu, pakawepo na njaa kuu nchi nzima. 26 Lakini Eliya hakutumwa kumwokoa hata mmojawapo wa hawa wajane, isipokuwa alitumwa kwa mjane mmoja wa kijiji cha Sarepta katika nchi ya Sidoni. 27 Na pia wakati wa nabii Elisha, walikuwepo wakoma wengi katika Israeli; lakini hakumtakasa hata mmoja wao, ila Naamani ambaye alikuwa raia wa Siria.”

Siria.”

28 Watu wote katika sinagogi waliposikia maneno haya, waka kasirika sana. 29 Wakasimama wote wakamtoa nje ya mji hadi kwe nye kilele cha mlima ambapo mji huo ulijengwa ili wamtupe chini kwenye mteremko mkali. 30 Lakini yeye akapita katikati yao akaenda zake. Yesu Afukuza Pepo Mchafu

31 Kisha akaenda Kapernaumu, mji ulioko wilaya ya Galilaya, na siku ya sabato akawafundisha watu katika sinagogi. 32 Walis taajabishwa na mafundisho yake, maana maneno yake yalikuwa na mamlaka. 33 Alikuwepo mtu mmoja katika sinagogi aliyekuwa ame pagawa na pepo mchafu, naye alianza kupiga kelele kwa nguvu akisema, 34 “Unataka kutufanya nini, Wewe Yesu wa Nazareti? Ume kuja kutuangamiza? Nakufahamu wewe ni nani. Wewe ni Mtakatifu wa Mungu.” 35 Yesu akamwamuru yule pepo: “Nyamaza! Mtoke!” Yule pepo akamwangusha chini yule mtu mbele yao, akamtoka pasipo kumd huru. 36 Watu wote wakashangaa wakaambiana, “Mafundisho ya mtu huyu ni ya ajabu. Anawaamuru pepo wachafu kwa mamlaka na nguvu, nao wanatoka! 37 Habari zake zikaenea pote katika mkoa ule.

Yesu Awaponya Wengi

38 Alipotoka katika sinagogi Yesu alikwenda nyumbani kwa Simoni na alipofika huko alimkuta mama mkwe wa Simoni ana homa kali. Wakamwomba sana amponye. 39 Basi Yesu akasimama kando ya kitanda chake akaiamuru ile homa imtoke. Homa ikamtoka yule mama. Akaamka mara moja akaanza kuwahudumia. 40 Jua lilipokuwa likichwa, wote waliokuwa na wagonjwa wenye maradhi mbalimbali waliwaleta kwa Yesu. Akamgusa kila mgonjwa, akawaponya wote. 41 Pepo wachafu pia waliwatoka watu wengi, nao walipokuwa wakitoka wakapiga kelele wakisema: “Wewe ni Mwana wa Mungu!” Lakini Yesu akawakemea na kuwazuia wasiseme, kwa maana walifahamu kuwa yeye ni Kristo.

42 Kesho yake, kulipopambazuka, Yesu alikwenda mahali pa faragha. Watu wengi wakawa wanamtafuta kila mahali, na walipom wona wakajaribu kumzuia asiondoke. 43 Lakini yeye akawaambia, “Ninao wajibu wa kuhubiri Habari Njema za Ufalme wa Mungu sehemu nyingine pia. Hii ndio sababu nilitumwa.” 44 Kwa hiyo akaende lea kuhubiri katika masinagogi ya Yudea. Yesu Awachagua Wanafunzi Wa Kwanza