Maagizo Ya Mwisho

Ninakuamuru mbele za Mungu na mbele za Kristo Yesu ambaye atawahukumu walio hai na wafu; na kwa kuja kwake na ufalme wake: hubiri Neno; lisisitize wakati ufaao na wakati usiofaa; sadik isha, kemea, na kuonya kwa uvumilivu mkuu na mafundisho thabiti. Maana wakati unakuja ambapo watu hawatavumilia kusikia mafund isho yenye uzima; bali kwa kuzifuata nia zao wenyewe watajilundi kia walimu tele watakaowaambia yale ambayo masikio yao yanatamani sana kuyasikia. Watakataa kabisa kusikia kweli na watageukia hadithi za uongo. Bali wewe uwe imara, katika mambo yote, vumilia mateso, fanya kazi ya mhubiri wa Injili, timiza wajibu wote wa huduma yako.

Maana mimi sasa ni tayari kutolewa kama sadaka, saa ya kuondoka kwangu imefika. Nimepigana ile vita njema, nimemaliza shindano, nimeitunza imani. Na sasa nimewekewa taji ya haki ambayo Bwana, mwamuzi wa haki, atanituza Siku ile; wala si mimi tu, bali na wote ambao wamengojea kwa hamu kuja kwake.

Maombi Ya Binafsi

Jitahidi kuja kuniona upesi 10 kwa sababu Dema, kwa kuu penda ulimwengu huu wa sasa, ameniacha akaenda Thesalonike. Kreske amekwenda Galatia na Tito amekwenda Dalmatia.

11 Ni Luka peke yake ambaye yupo hapa pamoja nami. Mchukue Marko uje pamoja naye kwa sababu ananisaidia katika huduma yangu. 12 Nimemtuma Tikiko Efeso. 13 Utakapokuja, niletee lile joho nililoliacha kwa Karpo huko Troa na vile vitabu, hasa vile vya ngozi.

14 Aleksanda mfua chuma alinitendea ubaya mkubwa. Mungu atamlipa kwa yale aliyonitendea. 15 Wewe pia ujihadhari naye kwa sababu alipinga vikali ujumbe wetu.

16 Nilipojitetea mara ya kwanza hakuna hata mmoja aliyekuwa upande wangu, kila mmoja alinikimbia. Naomba wasihesabiwe hatia kwa jambo hilo. 17 Lakini Bwana alisimama nami akanitia nguvu kutangaza Habari Njema kwa ukamilifu ili watu wote wa mataifa wapate kusikia. Na niliokolewa kutoka katika kinywa cha simba. 18 Bwana ataniokoa katika kila uovu na kunihifadhi mpaka niu fikie ufalme wake wa mbinguni. Atukuzwe Yeye milele na milele.

Salamu Za Mwisho

19 Nisalimie Prisila na Akila na wote waliomo nyumbani kwa Onesiforo. 20 Erasto alibaki Korintho. Trofimo nilimwacha akiwa mgonjwa huko Mileto.

21 Jitahidi kufika huku kabla ya majira ya baridi kali. Sal amu zako kutoka kwa Eubulo, Pude, Lino, Klaudia na ndugu wote.

Nakuamuru mbele za Mungu na mbele za Kristo Yesu, ambaye punde atawahukumu wale walio hai na wale waliokwisha kufa na juu ya kuja kwa mara ya pili kwa Kristo kwa sababu kwa hakika atatokea kuja kutawala kama Mfalme: Hubiri Ujumbe, uwe tayari kutimiza wajibu wako wakati ulio sahihi hata ule usio sahihi. Wathibitishie watu kwa wanafanya makosa na uwaonye juu ya yale yatakayowatokea. Ufanye hivi kwa subira kubwa na tahadhari katika yale unayofundisha.

Nasema hivi kwa sababu utakuja wakati ambapo watu hawatakuwa tayari kuyasikiliza mafundisho yenye uzima. Badala yake watawatafuta walimu wanaowapendeza. Watawatafuta walimu wanaosema yale wanayotaka kusikia. Na watayageuzia mbali masikio yao kutoka kwenye kweli na kugeukia simulizi za uongo. Lakini wewe ujizuie mwenyewe katika mambo yote; vumilia mateso; fanya kazi ya mhubiri wa Habari Njema; ifanye huduma uliyopewa na Mungu.

Kwangu mimi, nimemiminwa kama kinywaji cha sadaka, na wakati wa kuondoka kwangu kutoka katika maisha haya umekwisha kufika. Nimejihusisha katika mashindano ya thamani; nimemaliza mbio; nimeilinda imani. Sasa tuzo ya mshindi inaningoja, hii ni taji inatolewa kwa wenye haki. Bwana, aliye hakimu wa haki atanipa taji hiyo katika Siku ile. Ndio atanipa mimi na yeyote mwingine anayengojea kwa dhati kuja kwake.

Maelezo Binafsi

Jitahidi kuja kuniona mapema uwezavyo, 10 kwani Dema aliniacha kwa sababu aliupenda ulimwengu wa sasa na ameenda Thesalonike. Kreske ameenda Galatia, na Tito ameenda Dalmatia. 11 Luka ni peke yake aliyebaki nami. Mchukue Marko na uje naye utakapokuja, kwa sababu anaweza kunisaidia katika kazi yangu. 12 Namtuma Tikiko kule Efeso.

13 Utakapokuja njoo na koti nililoliacha katika nyumba ya Karpo kule Troa. Pia uniletee vitabu vyangu, hasa vile vya ngozi.

14 Iskanda aliye mfua vyuma amenitendea mabaya mengi. Bwana atamlipa kwa yale aliyotenda. 15 Wewe pia uwe mwangalifu kwake, kwa kuwa ameyapinga kwa juhudi mafundisho yetu.

16 Mara ya kwanza nilipokuwa nafanya utetezi wangu, hakuna hata mmoja aliyekuja kunisaidia. Badala yake wote wakaniacha. Na wasihesabiwe hayo na Mungu. 17 Lakini Bwana akasimama upande wangu na kunitia nguvu, ili ujumbe uweze kunenwa nami kwa ukamilifu ili kwamba Mataifa wote waweze kusikia. Na nikaokolewa kutoka katika mdomo wa simba. 18 Bwana ataniokoa kutokana na kila mashambulizi maovu na atanileta salama katika Ufalme wake wa mbinguni. Utukufu uwe wake milele na milele. Amina.

Salamu za Mwisho

19 Msalimu Priska na Akila na wale wa nyumbani mwake Onesiforo. 20 Erasto alibaki Korintho. Nilimwacha Trofimo kule Mileto kwa sababu alikuwa mgonjwa. 21 Jitahidi kuja kabla ya msimu wa baridi.

Ebulo anakusalimu, na Pude, Lino, na Klaudia, na ndugu na dada wote.

22 Bwana awe nawe. Neema ya Mungu iwe nanyi.